Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Saturday, June 14, 2014

Jaji Mwesumo: Aboud Jumbe alisababisha niache kazi

Wahenga walisema, kila zama na kitabu chake, ndivyo ilivyo siyo tu kwa watawala, bali hata maisha ya kila mwanadamu yana ‘kitabu chake.’
Hilo linaweza kuthibitishwa na mambo mbalimbali, lakini kwa namna ya pekee historia ya Mwanasheria, aliyekuwa pia Mbunge, Naibu Waziri na sasa mkulima, Jaji Mstaafu Edward Mwesumo.
Katika mahojiano na Mwananchi Jumamosi, Jaji Mwesumo ambaye sasa anaishi eneo la Sagamaganga, Ifakara katika Wilaya ya Kilombero mkoani Morogoro anaeleza mengi yaliyomkumba wakati wa zama zake za utumishi, akiwa amebahatika kuhudumu mihimili mitatu ya dola ambayo ni Mahakama, Bunge na Serikali.
Alianza utumishi mwaka 1962 katika iliyokuwa Wizara ya Ardhi, Maliasili na Wanyama wakati huo akiwa karani.
Anasema baada ya miezi minne kazini, alijiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na mwaka 1965 alihitimu Shahada ya Sheria. Mwaka 1966 aliajiriwa na Serikali na kufanya kazi ya uhakimu katika mikoa ya Dar es Salaam, Arusha, Singida, Tanga na Dodoma hadi mwaka 1971.
“Nilifanya kazi katika idara ya Mahakama kwa ngazi tofauti hadi kuwa Jaji wa Mahakama tangu mwaka 1966 hadi mwaka 1980,” anasimulia Jaji Mwesumo.
Kesi anayokumbuka
Akizungumzia utendaji wake katika idara ya Mahakama iliyo na kazi ya kutafsiri sheria, Jaji Mwesumo anasema anakumbuka mambo mengi mazuri, lakini moja kubwa ni kesi ambayo mwishowe ilisababisha yeye kuondoka kwenye nafasi ya ujaji aliyokuwa nayo.
Anasimulia kuwa tukio hilo lilitokea mwaka 1979 aliposimamia kesi ya kwanza ya kikatiba nchini katika Mahakama Kuu mkoani Arusha.
“Nakumbuka wakati huo Rais wa Zanzibar na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano, Aboud Jumbe aliwaweka watu kizuizini. Wakati huo mimi  kituo changu cha kazi kilikuwa Arusha na bosi wangu alikuwa Jaji Nassoro Mnzava.
“Happy Makole na Wamasai watatu waliwekwa kizuizini kwa amri ya Rais Jumbe ambaye alisema kuwa watu hao ni hatari kwa nchi.
“Watu hao waliweka mawakili watatu, walikuwa ni James Mwale na wenzake ambao walifungua kesi kupinga amri hiyo ya Rais. Bosi wangu, Mnzava akanipangia kesi hiyo, niliisikiliza kwa hatua mbili.
Kwa habari zaidi ingiahttp://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/Jaji-Mwesumo--Aboud-Jumbe-alisababisha-niache-kazi/-/1597296/2348056/-/5e8wwq/-/index.html
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment