Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Tuesday, May 6, 2014

Rais Kikwete aahidi Serikali kuajiri mahakimu 600


Jaji Mkuu Mohamed Othman Chande akizungumza na mmoja wa majaji wanawake ambao wanakutana katika mkutano wa siku nne jijini Arusha. Picha na Mussa Juma 
Na Mussa Juma, MwananchiArusha. Rais Jakaya Kikwete amesema serikali inakusudia kuboresha utendaji wa mahakama nchini kwa kuongeza ajira na kuendelea kufanyia mabadiliko sheria ambazo zimepitwa na wakati.
Kwa kuanzia, Rais alisema katika siku chache zijazo Serikali itaajiri mahakimu 600 wa mahakama mbalimbali ili kupunguza upungufu wa watumishi hao.
Akifungua Mkutano Mkuu wa Kimataifa wa Majaji Wanawake Duniani (IAWJ) jijini hapa, Rais Kikwete alisema kutokana na upungufu wa watendaji wa mahakama na mahitaji mengine, wananchi wengi hasa maskini na wanawake, wanakosa haki zao.
“Serikali ina mikakati kadhaa ya kuhakikisha inaboresha sekta ya mahakama nchini ili kuhakikisha wananchi wanapata haki kwa wakati,” alisema
Aliwataka majaji wanawake kuendelea kusaidia upatikanaji wa haki kwa wakati ili kuondoa matatizo ya kesi kusikilizwa kwa muda mrefu.
Awali rais wa Chama cha Majaji Wanawake Duniani, Jaji wa Rufaa Mstaafu Eusebia Munuo alisema kaulimbiu ya mkutano huo ni kutolewa haki kwa usawa kwa wananchi wote.
Alisema utoaji wa haki kwa usawa ni suala la utekelezwaji wa haki za binadamu na akatoa wito kwa majaji wanawake kusaidia wananchi kupata haki zao.
Akizungumza mapungufu ya sheria, alitaka kuunga mkono jitihada za serikali ya Tanzania kuendelea kufanya mabadiliko ya sheria hasa ambazo zimepatwa na wakati.
Alisema mkutano huo ambao umewashirikisha majaji zaidi ya 600 umeandaliwa kwa pamoja na IAWJ na Chama cha Majaji Wanawake Tanzania (TAWJA).
Mkutano huo wa siku nne unafanyika kwa mara ya kwanza nchini tangu chama hicho kianzishwe mwaka 1991.
Jaji Munuo alisema, mkutano huo unashirikisha majaji zaidi ya 600 wanawake kutoka nchi mbalimbali duniani wakiongozwa na rais wa chama hicho.
Alisema mkutano huo utatoa fursa ya kupanua wigo wa mawasiliano kati ya majaji wanawake ili kujenga mazingira mazuri ya utendaji kazi pamoja na kujenga ubora na uadilifu katika utoaji wa haki na ukuzaji wa haki za binadamu.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment