Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Thursday, May 8, 2014

Nigeria:Polisi waahidi dola laki 3

 
Kundi la Boko Haram limekiri kuwateka nyara wasichana hao na kusema kuwa litawauza
Polisi nchini Nigeria wameahidi kumtunuku dola laki tatu za marekani yeyote atakayetoa habari zitakazowasaidia kuwapata zaidi ya wasichana mia mbili waliotekwa na kundi la wapiganaji wa boko haram mwezi uliopita .
Juma lililopita Wapiganaji wa Boko Haram walisema kuwa wasichana hao 200 kutoka eneo la Chibok waliotekwa mwezi uliopita watauzwa.
Aidha Maafisa nchini Nigeria Wamesema kuwa idadi ya wasichana zaidi waliotekwa nyara na kundi la wapiganaji wa kiislamu wa Boko Haram imetimu 11.
8 kati yao walitekwa kutoka kijiji cha Warabe kilichoko katika jimbo la Borno siku ya jumapili nao watatu zaidi wakatekwa kutoka kijiji jirani .
Rais wa Marekani ameingilia swala hilo akisema kuwa serikali yake itatoa msaada ili kuwakomesha wapiganaji hao.
Tayari marekani imewatuma maafisa kadhaa kusaidia kusuluhisha kwa amani kitendawili cha utekaji nyara huo.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment