Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Friday, May 9, 2014

MCHUNGAJI AFARIKI DUNIA, WIKI TANO BAADA YA SHUKRANI KWA MUNGU KWAMBA KANISA HALIJAWAHI KUPATA MSIBA


Marehemu mchungaji DB Antrim akiwa na mmoja wa watoto wake.©Facebook/ DB Antrim.
Huzuni kubwa imelikumba kanisa la Westwind eneo la Waukee huko IOWA nchini Marekani baada ya kujiua kwa mchungaji mmojawapo wa kanisa hilo ikiwa ni wiki tano kupita toka mchungaji kiongozi Brandon Barker kumshukuru Mungu kwamba zaidi ya miaka mitano katika historia ya kanisa hilo hawajapatwa na msiba wa muumini au kiongozi kufa.

Kwa mujibu wa daktari aliyekuwa akiuchunguza mwili wa mchungaji DB Antrim ametangaza kutokea kutokea kwa kifo cha mchungaji huyo aliyeacha watoto wawili wa kiume na mke mmoja bila kufafanua hasa chanzo cha kifo chake. Kwa upande wake mchungaji Barker akizungumza kwa huzuni
Mke wa marehemu Allison Sherwood Antrim na mtoto wao.
kanisani jumapili iliyopita, alisema kwamba kanisa hilo linapitia kipindi kigumu kisichoelezeka kutokana na kifo cha mchungaji Antrim ambaye amesema amejiua kwa mikono yake mwenyewe, na kwamba kifo hicho hakitasahaulika katika uhai wake.

Mchungaji Barker amesema ilikuwa vigumu kukubali kwamba Antrim amefariki siku ya alhamisi iliyopita kutokana kwamba masaa machache nyuma walikaa pamoja kuzungumzia ujumbe atakaohubiri marehemu siku ya jumapili na kwamba hakuwa na wazo kwamba siku hiyo ingeisha vibaya na kuwaachia maumivu makubwa kwakuwa alishuhudia kwa macho yake mwili wa mchungaji Antrim.

Watoto wa marehemu mchungaji Antrim.          
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment