Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Tuesday, May 6, 2014

Marekani yatambua rasmi waasi wa Syria

 
 Hawa ni baadhi ya viongozi wa waasi wa Syria waliopewa hadhi maalumu nchini Marekani.
Marekani imewapa waasi wa Misri hadhi ya kidiplomasia ambapo wamefungua afisi nchini humo.
Hatua hiyo ilitangazwa wakati wajumbe wa muungano wa waasi walipowasili mjini Washington katika ziara yao rasmi ya kwanza nchini humo.
Hata hivyo Marekani haitambui muungano wa waasi hao wa Syria kama Serikali ya taifa lao na wala hawaruhusiwi kuingia katika ubalozi wa Syria.
Maafisa wa Serikali ya Marekani walisema hatua hiyo imechukuliwa kama hatua ya kujaribu kuimarisha uhusiano na upande wa upinzani wenye msimamo wa kadiri.
Hatua hii itasaidia huduma za benki na usalama, na wakati huohuo kusaidia makundi ya upinzani kuimarisha sifa ya Marekani miongoni mwa raia wa Syria wanaoishi ng'ambo.
Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Marekani imetangaza msaada zaidi wa Dola milioni 27 kwa muungano huo wa waasi.
Hadi kufikia sasa Marekani imeendelea kutoa misaada isiyo ya silaha ingawa baadhi ya maafisa Serikalini wamependekeza kuwa msaada wa kijeshi uanze kutolewa kwa waasi hao.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment