Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Thursday, May 22, 2014

Magufuli akumbuka barabara 10

Dodoma. Wizara ya Ujenzi imetenga Sh28.94 bilioni kwa ajili ya kutekeleza miradi ya kujenga, kufanya upanuzi na kukarabati barabara 10 za mchepuko katika Jiji la Dar es Salaam ili kupunguza msongamano wa magari.
Akiwasilisha bajeti ya wizara yake kwa mwaka 2014/2015 bungeni Dodoma juzi jioni, Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli alisema mradi huo utahusisha barabara zenye urefu wa kilometa 109.35.
Barabara zitakazohusika katika mradi huo ni Kawawa kwenda Bonde la Msimbazi hadi makutano ya Jangwani na Twiga ambayo itakuwa na urefu wa kilometa 2.7.
Nyingine ni Jet Corner kwenda Vituka hadi Devis, kilometa 10.3, sehemu ya Tabata Dampo kilometa 2.25 na Kimara –Kilungule – External, kilometa tisa.
Barabara nyingine ni Mbezi - Marambamawili – Kinyerezi –Banana, kilometa 14, Tegeta – Kibaoni - Wazo Hill - Goba hadi Mbezi, Barabara ya Morogoro ambayo itakuwa na urefu wa kilometa 20.
Nyingine ni Tangi Bovu - Goba kilometa tisa, Kimara – Baruti - Msewe, Kibamba - Kisopwa, Banana - Kitunda-Kivule – Msongola, kilometa 14.7.
Mradi huo unahusisha pia barabara nyingine ya Ardhi - Makongo yenye urefu wa kilometa 4 na mradi wa ujenzi wa miundombinu ya mabasi yaendayo haraka na vituo vyake unaoendelea
Fedha zilizotengwa
Dk Magufuli alisema Serikali imetenga Sh605 milioni kukamilisha kazi zilizobakia kwa Barabara ya Kawawa - Msimbazi na makutano ya Jangwani na Twiga.
Pia alisema Sh1.29 bilioni zimetengwa kulipa sehemu ya madai kwa ajili ya mkandarasi anayejenga Barabara ya Jet Corner - Vituka hadi Devis Corner.
Pia Waziri huyo alisema Serikali imetenga Sh2.5 bilioni kwa ajili ya kuanza ujenzi wa Barabara ya Ubungo – Maziwa - External na Tabata Dampo - Kigogo.
Mbali na bajeti hiyo, alisema Serikali pia imetenga Sh5 bilioni kwa ajili ya kuanza ujenzi wa Barabara ya Kimara – Kilungule - External na Sh6 bilioni kwa ajili ya Mbezi – Marambamawili - Kinyerezi hadi Banana.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment