Latest News

GNM Cargo

GNM Cargo
GNM CARGO & LOGISTICS

menu

Sunday, January 26, 2014

Hakuna aliyesitisha mapigano Sudan-K

Serikali ya Sudan Kusini na wapiganaji wanaendelea kulaumiana kwa kuvunja makubaliano ya kusitisha mapigano ambayo yalianza kutekelezwa Ijumaa.
Wanajeshi wa serikali ya Sudan Kusini
Msemaji wa waasi, Brigedia Jenerali Lul Ruai, alieleza kuwa wanajeshi wa serikali wameshambulia maeneo yao katika sehemu kadha.
Serikali ilikanusha hayo na iliwalaumu waasi kwa mashambulio.
Kila upande unasema haufikiri kuwa upande wa pili unaweza hasa kudhibiti majeshi yake.
Maelfu ya watu wamekufa katika vita hivyo baina ya jeshi la serikali ya Rais Salva Kiir na wanajeshi watiifu kwa naibu wake wa zamani, Riek Machar.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment