Latest News

GNM Cargo

GNM Cargo
GNM CARGO & LOGISTICS

menu

Tuesday, December 10, 2013

Dakika za mwisho za maisha ya Mandela

Huku bunge la afrika kusini likifanya kikao maalum cha kumheshimu mandela ,mwanawe mkubwa wa kike Makaziwe ameiambia BBC kuhusu dakika za mwisho za maisha ya babake.
Mwanawe Mandela Makaziwe Mandela
Amesema kuwa ijapokuwa hakuwa akifungua macho mara kwa mara,alikuwa na uhakika kuwa aliweza kusikia vile familia yake ilivyompenda.
Makaziwe amekiri kuwa hakuweza kuwasiliana vyema sana na babake na kwamba babake hakuweza kuonyesha hisia zake,lakini yote hayo alitaka familia yake kupatana.
Amesema kitu kikubwa alichoelimishwa na babaake ni kuwa na ujasiri wa kusamehe.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment