Latest News

GNM Cargo

GNM Cargo
GNM CARGO & LOGISTICS

menu

Wednesday, August 14, 2013

Viongozi wa dini watakiwa kutokujihusisha na siasa

Igunga. Mkuu wa Wilaya ya Igunga, mkoani Tabora, Elibariki Kingu, amewaasa viongozi wa dini kutokujihusisha na masuala ya siasa, badala yake wajenge misingi ya kiroho kwa waumini.
Akizungumza kwenye tamasha la uzinduzi wa albamu ya nyimbo za Injili ya Anna Nzogi, Kingu alisema baadhi ya viongozi wa dini wamekuwa wakijihusisha na siasa na kuacha kumtumikia Mungu, hali ambayo inaleta vurugu.
Kingu alisema baadhi ya wananchi wamekuwa wakitumia fedha nyingi kufanya mambo yasiyompendeza Mungu, badala ya kuwekeza kwa shughuli mbalimbali za maendeleo na kutoa sadaka na kwamba, watumie uwezo wa Mungu aliowajalia. 
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment