Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Sunday, August 11, 2013

MALI:UCHAGUZI WA MARUDIO

 Wagombea urais,Soumaila Cisse,(Kushoto) na Boubacar Keita, (Kulia)
             Wagombea urais,Soumaila Cisse,(Kushoto) na Boubacar Keita, (Kulia)
Kampeni zimekamilika nchini Mali kabla ya uchaguzi wa marudio Jumapili. Wagombea  wawili wa kiti cha rais walifuta mikutano  ya hadhara Ijumaa kuadhimisha mwisho wa mwezi wa Ramadhan, mwezi mtukufu kwa Waislam.

Mgombea Ibrahimi Boubacar Keita ambaye anaonekana kuwa na na nafasi nzuri katika uchaguzi huu  ameahidi kurejesha amani katika taifa hilo la Afrika Magharibi ambalo limedumazwa na mapinduzi ya serikali yaliyofanywa na majeshi na wimbi la  maasi ya wanamgambo kutoka  upande wa kaskazini mwa nchi.

Keita alipata asili mia 40 ya kura katika duru ya kwanza  ya uchaguzi mwezi jana dhidi ya mpinzani wake wa karibu Soumalia Cisse ambaye zamani alikuwa waziri wa fedha.

Cisse alidai kulikuwa na wizi wa kura katika duru ya kwanza ya uchaguzi  lakini amesema atakubali matokeo ya uchaguzi wa Jumapili.

Atakayeshinda uchaguzi huu ana muda wa miezi miwili kuanza mazungumzo na waasi wa Tuareg wanaopigana kujitenga na Mali upande wa kaskazini mwa nchi, kama sehemu ya makubaliano ya sitisho la mapigano na serikali lililofikiwa mwezi Juni.


Imewekwa na Happy Adam
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment