UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

Sunday, August 11, 2013

KKKT DAYOSISI YA IRINGA USHARIKA WA KIHESA WAZINDUA ALBAMU

Kwaya ya watoto waliokatika malezi maalum kupitia shirika liitwalo Compasion katika  Ushirika wa Kihesa wamefanikiwa kuzindua albamu yenye nyimbo 9 inayokwenda kwa jina la ‘WAMTUMAINIO BWANA’.
Uzinduzi huo umefanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Chuo cha Ualimu Kreluu na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali na Wachungaji wa Kanisa la Kilutheri liliko mjini Iringa.
Katika uzinduzi huo uliofanyika  huku  mgeni rasmi akiwa  mbunge wa viti maalum Lita Kabati ulifana kwa kwaya hiyo kuweza kuburudisha kwa nyimbo za kumsifu MUNGU na kuweza kuwateka mashabiki waliohudhuria
Katika uzinduzi huo Lita Kabati aliweza kuchangia kiasi cha shilingi milioni 1 albamu hiyo nyimbo za ‘Njooni kwangu, Chagueni,Twashukuru, Heri,Wamtumainio Bwana unaobeba jina la Albamu, Siendi kwa Shetani, Ninaye Yesu, Tazama na Baba.
Kwaya hiyo ilifungua na wimbo wa Tushukuru Muumba  uliopokelewa vyema na mashabiki na wimbo wa pili Nitaimba sifa zako kutoka katika albamu ya Wamtumainio Bwana iliyofanywa na studio za MBC-Hot media ya jijini Dar es salaam.
Wasanii waliosindikiza uzinduzi huo pamoja na Eunice Bujiku anayetamba na wimbo wake wa  ‘Fadhila za Bwana, Kwaya ya Uinjilisti Kihesa, Kwaya ya Usharika wa Kihesa, Kwaya ya Vijana-Kihesa  na na msanii wa nyimbo za dini anayekuja kasi  Atosha Kisava .
Mkuuwa Jimbo la Kaskazini Kihesa Mchungaji Donald Kiwanga alisema wakati wa kumkaribisha mgeni rasmi kuwa lengo la kuzindua albamu hiyo ni kuweza kupata mapato ambayo yataweza kuwasaidia wanakwaya hao kuboresha makazi yao na matumizi ya Kanisa la MUNGU.

Mpaka mwisho zaidi ya milioni sita zilikuwa zimepatikana ikiwa ni fedha taslim na ahadi 
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment