Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Monday, April 9, 2018

Adhabu ya Kifo Mali, yashutumiwa

Mlinzi wa amani nchini Mali, akilinda usalama

Haki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionMlinzi wa amani nchini Mali, akilinda usalama
Kikundi cha kutetea haki za binaadamu nchini Mali kimeshusha mzigo wa lawama kwa jeshi la nchi hiyo kutokana na kitendo cha kutekeleza adhabu ya kifo kwa wafungwa kumi na wanne katikati mwa jiji la Dioura.
Jeshi la nchi hiyo liliarifu kuwa wafungwa hao walikamatwa Almamisi wiki iliyopita na kuuawa muda mfupi tu baadaye.
Ndugu wa marehemu, ambao wanatoka katika kundi la kabila la Fulani, wametoa maelezo kuwa, ndugu zao hawakuwa na nasaba yoyote na makundi ya vijana wenye msimamo mkali.
Jamii hiyo ya kabila la Fulani imelalamika kuwa hii si mara ya kwanza kuhusishwa na makundi yenye msimamo mkali wa kidini.
Wiki hii, harakati za kundi la haki za binaadamu la Amnesty International limearifu kuwa wanaume sita walikutwa wamekufa katika kaburi la halaiki mapema mwezi uliopita ambao walitiwa mikono na jeshi siku tatu nyuma.
BBC
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment