Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Tuesday, February 4, 2014

Polisi watawanya wachimba migodi A.Kusini

Polisi nchini Afrika Kusini wametumia maguruneti na risasi za mipira kuwatawanya zaidi ya wachimba migodi ambao walikuwa wanaandamana karibu na mji wa Rustenburg.
Wachimba migodi wamekuwa wakiandamana kutaka nyongeza ya mishahara
Polisi wanasema kuwa wachimba migodi hao katika mojawpao ya migodi ya kampuni ya Anglo-American,walikuwa wanabeba silha hatari na kutishia kuwaondoa wafnyakazi wenzao kutoka mgodini.
Polisi wamewakamata watu wawili.
Takriban wanachama elfu nane wa muungano wa wachimba migodi na wajenzi walifanya mgomo mnamo mwezi january wakitaka kuongezwa mshahara.
Mgomo huo ni mkubwa zaidi kuwahi kufanyika nchini Afrika ya kusini katika sekta ya uchimbaji wa madini ya platinum tangia mgomo wa mgodi wa marikana mnamo mwaka 2012 ambapo maafisa wa polisi waliwapiga risasi na kuwauawa wachimba mgodi 34.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment