Writen by
sadataley
10:20 PM
-
0
Comments
Awali Shirika hilo lilitoa taarifa ya kuuwawa kwa watu thelathini na sita wakiwemo watoto kumi na tano. Taarifa hio haijathibitisha iwapo kuna waasi waliouwawa
Waangalizi wa Haki za Binadamu wanasema mauaji hayo yametokana na mashambulizi yaliyotekelezwa katika wilaya zinazodhibitiwa na waasi.
Mashambulizi hayo yamekuja siku moja baada ya Shirika la Msalaba mwekundu kufikisha msaada wa chakula na dawa katika gereza moja ambalo limekuwa chini ya udhibiti wa waasi kwa takribani miezi nane.
Vikosi vya serikali vimekuwa vikifanya mashambulizi hayo kuwalenga waasi, lakini hata wale wasiokuwa na hatia wamekuwa wakiathiriwa.
Mamilioni ya raia wa nchi hiyo wameendelea kukimbia makazi yao, huku watu zaidi ya laki moja na ishirini wakiuawa toka kuanza kwa mapigano hayo miezi thelathini na tatu iliyopita.
No comments
Post a Comment