Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Tuesday, December 17, 2013

Tunisia:Tumechoshwa na serikali

Maelfu ya watu nchini Tunisia wamekuwa wakifanya maandamano mjini Sidi Bouzid, kitovu cha harakati za mapinduzi ya kiraia yaliyomwondoa mamlakani aliyekuwa Rais Zine el-Abidine Ben Ali miaka mitatu iliyopita.
Wengi wanasema serikali inajikokota kupiga hatua tangu mapinduzi ya kiraia
Waandamanaji wanalalamikia ukosefu wa serikali kupiga hatua za kuridhisha tangu mapinduzi ya kiraia kufanyika.
Mji wa Sidi Bouzid ndiko kijana mmoja mchuuzi Mohamed Bouazizi alijiteketeza miaka mitatu iliyopita kuonyesha ghadhabu kwa ambavyo serikali ilikuwa inawanyanyasa raia wake.
Maandamano yaliyofuata tukio la kijana huyo kujiua, yalimwondoa mamlakani aliyekuwa Rais Zine el-Abidine Ben Ali na kuchochea maandamano mengine kama hayo katika nchi za kiarabu.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment