Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Saturday, December 21, 2013

Kikwete afukuza mawaziri wanne TZ

Rais wa Tanzania amewafukuza kazi mawaziri wanne baada ya kutengua uteuzi wao kwa tuhuma za kushindwa kusimamia operesheni ya kuwasaka majangili.
Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete
Hatua hii ya Rais Kikwete ya kutengua uteuzi unatokana na shinikizo la Bunge la Tanzania ambao walitaka mawaziri hao wajiuzulu wenyewe au rais awafukuze kazi kutokana matukio ya mauaji, utesaji na uvunjifu wa haki za binadamu wakati wa operesheni hiyo uliofanywa na watendaji walio ndani ya wizara zao.
Mauaji, utesaji na ukiukaji wa haki za binadamu wakati operesheni ulifichuliwa na taarifa ya kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na utalii iliyopewa jukumu ya kufanya uchunguzi baada ya kuwepo kwa malalamiko kuwa operesheni hiyo uliambatana na ukiukaji wa haki za binadamu.
Miongoni mwa mateso na ukiukwaji wa haki za binadamu uliotajwa kwenye ripoti ya kamati hiyo ilikuwa ni mauaji, utesaji ikiwemo kuwalazimisha baadhi ya wanaume kufanya mapenzi na miti au wanyama waliokufa.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment