Writen by
sadataley
9:14 PM
-
0
Comments
Hayo yaliombwa jana na Papa Francis katika misa aliyoongoza kwamba yeye na wafuasi wengine ambao ni Majesuiti watapokea 'Aibu yenye neema ndani yake' katika mapungufu yao na katika unyenyekevu wao hakuna awezaye kuyatambua isipokuwa Kristo Yesu pekee.
Papa Francis akiwa anatoka nje ya kanisa la Gesù huko Roma
Yesu aliwaambia wanafunzi wake kamwe wasipatwe na aibu pale waamuapo kumfuata, lakini Majesuiti hufundishwa juu ya kuutazama msalaba na kuacha mambo mengine yote ya ulimwenguni "kujisikia kwamba kuwa binadamu au mheshimiwa ni heshima ya duniani tu ambayo ina kiomo hapahapa duniani na si mbinguni", Papa alisema wakati wa hotuba yake katika Misa katika huko Roma katika kanisa la Gesù,katika sikukuu ya Mtakatifu Ignatius. Na pia kuwa Mtakatifu ni kuzikwa ndani yakanisa.
Msemaji wa Vatican Padre Federico Lombardi SJ alisema Misa ilikuwa "nzuri sana na ya kifamilia". Katika mapokeo yake ya kiroho, alisema, Papa anaonekana kama "mwana wa Mtakatifu Ignatius" na anahisi "kuwa Papa Francis hupenda sana kuwa karibu na jamii ya Yesu".
kwahabari zaidi tembelea;http://www.catholicherald.co.uk/news/2013/08/01/we-must-ask-for-the-grace-of-shame-pope-francis-tells-fellow-jesuits/
Imewekwa na Happy Adam
No comments
Post a Comment