Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Friday, July 28, 2017

Twaweza: Nusu ya Watanzania wako salama



UTAFITI uliofanywa na taasisi ya Twaweza umeonyesha kuwa usalama kwa nusu ya Watanzania umeimarika katika mwaka mmoja uliopita kwa asilimia 53 ambapo asilimia 37 walisema hali ya usalama imebaki vilevile na asilimia 10 wanasema hali imekuwa mbaya zaidi.
\
Utafiti huo umetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Twaweza, Aidan Eyakuze, katika mkutano na wadau uliofanyika katika Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa Dar, alipofafanua kuwa matokeo hayo yametokana na utafiti wake uitwao ‘Hapa usalama tu: Usalama, polisi na haki nchini Tanzania’.

“Muhtasari huu unatokana na takwimu zilizokusanywa kutoka sauti za wananchi, utafiti wa kwanza barani Afrika kwenye uwakilishi wa kitaifa unaotumia simu za mkononi.

Ni matokeo na takwimu zilizokusanywa kutoka kwa wahojiwa 1,805 katika maeneo mbalimbali ya Tanzania Bara bila kuhusisha serikali ya Zanzibar yaliyofanyika Aprili mwaka huu,” alisema.



« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment