Thursday, March 13, 2014

69 wauawa na wafugaji Nigeria

Mbunge mmoja anayewakilisha eneo hilo, Barrister Abdullahi Abbas Machika alisema kuwa watu 47 walizikwa hii leo katika kijiji kimoja katika jimbo la Katsina.
Duru kutoka katika hospitali ya Funtua,jimbo la Katsina, alisema kuwa angalau watu 15 wamelazwa hospitalini humo wakiwa na majeraha mabaya.
Wakazi wanasema kuwa hapakuwa na maafisa wa usalama, wakati wa shambulizi hilo tangu shambulizi lianze hapo jana.
Rais Goodluck Jonathan kwa sasa anazuru jimbo la Katsina kuzindua miradhi kadhaa ya maendeleo.
Mbunge anayewakilisha eneo hilo anadai kuwa maafisa wa usalama wanajishughulisha kumlinda Rais wakati raia wanauawa katika vijiji kadhaa.

No comments:

Post a Comment