Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

TAARIFA MBALIMBALI ZA KKKT-DIRA


TULIKOTOKEA......  

KANISA LA KWANZA  KUJENGWA-USHARIKA WA KWANZA KABISA 
MAARUFU "POMERN" POMERINI



 EVANGELICAL   LUTHERAN CHURCH IRINGA DIOCESE
ADDRESS
P.O. Box 511,
IRINGA.
Phone   +255 270 20 89
Fax       +255 270 11 98
Website   www.elctdira.org
IT’S ESTABLISHMENT
Iringa Diocese was established in 26th  September, 1987 with registration number SO.6906
VISION STATEMENT
“…I came that they may have life, and have it abundantly” (John 10:10b RSV)
MISSION STATEMENT
Iringa Diocese exists to witness, live in Christian fellowship and to serve the people created in the image of God Spiritually, Physically and Economically.
CORE VALUES
  • Evangelization
  • Christian nurture
  • Unity in Christ
  • Praise and worship
  • To identify and uphold the life of poor and oppressed
  • To work in partnership

LEADERSHIP
 Bishop                                      RT. REV. DR. OWDENBURG MOSES MDEGELLA
 Assistant to the Bishop          REV. BLASTON TULUWENE  GAVILE
 General secretary                 MR. NAYMAN CHAVALLA
 Treasurer                                 MR. NOEL     ILOMO


DEPARTMENTS
  • Planning and Development Department
  • Women and Family Nurture Department
  • Mission and Evangelism Department
  •  Christian Education and Youth Department
  • Theological Education by Extension Department
  • Communication and Information Department
  • Finance Department and
  • Building Department.
  • Training Unit
  •  Bega kwa Bega
  • Mission to Normadic Societies
  •  Malaria and
  • Pastors Spouses.
ON GOING PROJECTS
  • Iringa Hope SACCOS- linked with  Tumaini University where there are about 36 Congregations  has joined  SCCOS with the Capital of 120M
  • Malaria Projects
  • HIV/AIDS
  • Ujana Project
  • Afforestation  -Sponsored by  Lutheran Mission Cooperation (LMC)and
  • Agriculture Demonstration Plots-under Institute of Agriculture Tumaini university Iringa-BKB, Paythrum
  • Water project-St Paul Partners(SPP)-
  • Furaha News Paper-Comin Soon!
CHURCH DISTRICT
 The Diocese has Seven Church Districts namely;
  • Northern Church District (Kihesa)
  • Northwest Church District (Ilula)
  • Western Church District(Kanisa Kuu)
  • Southern west Church District (Ihemi)
  • Southern Church District(Pomerini)
  • Eastern Church  District (Ipalamwa) and
  •  Southern east Church District(Idete).
CONGREGATIONS
The Diocese has seventy nine  Congregations namely :-
  • SOUTHERN CHURCH DISTRICT(POMERINI)
Pommern,Lukani,Kitowo, Ihimbo, Bomalang’ombe, Masisiwe,Mwatasi,Ugesa,Kipanga,
Usokami and Ukumbi.
  • NORTHERN CHURCH DISTRICT (KIHESA)
Kihesa, Mlandege, MkimbiziNduli,ilambilole,Usolanga,Mtera,Mtwivila,Ikengeza,
Tumaini, Isimani and Migoli.
  • SOUTHERN WEST CHURCH DISTRICT (IHEMI)
Ihemi,Ipogolo,Magulilwa,Ifunda,Kiponzelo,Masimike,Wasa,Mgama nd Kitasengwa
  • NORTHWEST CHURCH DISTRICT (ILULA)
Ilula,Luganga,Kipaduka,Image,Itungi,Irindi,Mbuyuni,Nyanzwa,Uhominyi,
Mbigili and Ilambo.
  • SOUTHERN EAST CHURCH DISTRICT(IDETE).
Idete,Idunda,Muhanga,Kidabaga,MagomeNg’ang’ange,Kiwalamo,Idegenda,Wimbe,Itonya and Ndengisivili.
  • EASTERN CHURCH  DISTRICT (IPALAMWA)
 Ipalamwa, Makungu, Kising’a, Mlafu, Ifuwa, Lulanzi, Kimala and  Kilolo.
  • WESTERN CHURCH DISTRICT(KANISA KUU)
 Iringa Mjini, Mkwawa,Kitapilimwa, Pawaga, Kidamali,Tungamalenga, Mlowa, Magubike and Kiwele.
HEALTH
The Dioceses has Ilula Hospital which is Designated Hospital for Kilolo District and eight dispensaries;
  • Pommern  Dispensary
  •  Ideate Dispensary
  • Ipalamwa Dispensary
  •  Ruaha Mbuyuni
  •  Ihimbo Dispensary
  • Tungamalenga Dispensary and
  •  Image Dispensary.
  • Lulanzi-
  • Idunda-First aid
EDUCATION
The Diocese owns:-
  • Iringa University
  •  Ilula Nursing School at Ilula to be introduced soon
  • Pommern Secondary School at Pommern Village
  •  Lutangilo Secondary School at Idete
  • ,Image Secondary School at Image
  •  Bomalang’ombe Secondary School at Bomalang’ombe
  •  Ipalamwa Secondary School at Ipalamwa
  •  Mtera Secondary School  at Mtera and
  • Malecela Secondary School at Kidatu Morogoro 

HISTORIA YA KANISA LA KIINJILI LA KILUTHERI TANZANIA
Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) ni muungano waKilutheri katika nchi ya Tanzania. Mwaka 1938 makanisa saba yaKilutheri yaliungana kama Muungano wa Makanisa ya Kilutheri, na tarehe 19 Juni 1963 yalikuwa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania.
Lengo la KKKT ni kuwapa watu nafasi ya kumfahamu Yesu Kristo ili kupata maisha ya milele. Kanisa limejengwa juu ya msingi wa Yesu Kristo, limeongozwa na Neno la Mungu (Biblia) kama linapatikana katika Agano la Kale na Agano Jipya, na limeimarishwa katikasakramenti.
KKKT linaongozwa na Mkuu wa kanisa (askofu Mkuu) na maaskofu ishirini kutoka dayosisi ishirini, wakiwa na wanachama zaidi ya milioni .
Ofisi kuu wa KKKT imo katika mji wa Arusha. KKKT linalo uhusiano na All Africa Conference of Churches (AACC), Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT), Lutheran World Federation (LWF) na Lutheran Mission Cooperation (LMC).


SEHEMU YA HISTORIA YA  DAYOSISI YA IRINGA

Makabila yanayoishi katika eneo linalokaliwa na KKKT Dayosisi ya Iringa ni Wahehe ambao ni wengi kuliko makabila mengine, Wabena, wakinga na  wawanji.[1] Makabila mengine ni Wagogo, Wambugwa, Wasagala, Watiliti pamoja na makabila ya wahamiaji wakazi. Yapo pia makabila ya wafugaji waliohamia kwenye eneo hili, kama vile wamasai, wabarbaig na wasukuma.

KKKT Dayosisi ya Iringa ina historia inayorudi nyuma hadi mwaka 1899, mwaka ambapo Mmisionari wa Kijerumani Mch. Wilhelm Neuberg alianzisha stesheni mahali paitwapo itonya katika milima ya Udzungwa. Mchungaji huyu aliitwa na wenyeji wa eneo la Itonya kama “Mwambetani “kwa lugha ya kihehe ikimaanisha mnavuna nini? Hii ilitokea kwasababu kila alipohubiri alikuwa akiwauli mnavuna nini kutoka kwenye neno ninalo hubiri.[2] Kazi hii ya Injili iliyoanzishwa na Mch. Neuberg iliwezesha kutokea kwa sinodi ya Ubena-Uhehe mwaka 1902.

Chanzo halisi kilichosababisha Injili kuingia Itonya ni kwamba kulikuwa na mtu aliyeitwa Mwamagelanga mzaliwa wa maeneo ya Idete alikuwa anafanya kazi katika mashamba ya chai Lupembe huko Njombe. Mtu huyu aliamua kumuomba mmisionari mmoja kwa kumwambia kuwa watu wa maeneo ya Itonya wanahitaji Injili, ndipo mmisionari huyo aqliyeitwa Neuberg akawaambia wenzake na akakubali kupeleka Neno la Mungu katika maeneo ya Itonya. Inasadikiwa kuwa Wakristo wa kwanza kubatizwa walikuwa Aron Kikoti, Lupituko Mkemwa, Yehoswa Kikoti na ndio waliokuwa walimu na wahubiri wakiwa wanapata posho ya shilingi tano kwa mwezi.[3]

Stesheni nyingine ilianzishwa na Mch.Julius Oelke mahali paitwapo Ilutila katika milima ya Udzungwa pia. Stesheni hii ilipewa jina la Kijerumani liitywalo Neustettin, lenye maana ya ‘stesheni mpya’, hilo ni jina la mji mkuu wa eneo la Pommern katika Ujerumani ya Mashariki ya wakati ule na katika nchi ya Poland ya sasa.
Kufika mwaka 1930 mmisionari mwingine wa Kijerumani aitwaye Mch. Herman Neuberg mtoto wa Mch. Wilhelm Neuberg mwanzilishi wa stesheni ya Itonya alipewa wajibu wa kusimamia eneo la Kikanisa la Ubena-Uhehe na ulanga makao yake yakiwa pale Pommern katika nchi ya Wahehe mahali ambapo pia Herman Neuberg alizikwa baada ya kufariki mwaka 1969.[4]

Mch. Martin Nordfeldt kutoka Sweden, akisaidiana na Mch. Herbert Uhlin, alifika Ilula mwaka 1938. Nordfeldt na Uhlin walikuwa wametumwa na chama cha wamisionari cha SEM (Swedish Evangelical Mission). Kwenye utumishi wake Mchg Nordfeldt alishirikiana na mtumishi mwenyeji, Mch. Yohana Nyagawa aliyekuwa mkuu wa kanisa la Ubena –Uhehe mwaka1940 mpaka 1941. Juhudi za watumishi hawa ziliwezesha kuanza kwa ujenzi wa nyumba ya ibada katika stesheni ya Ilula pamoja na ujenzi wa shule ya Ilula iliyosimamiwa na na Mwl.Tulawona Luka. Baada ya hapo shule zaidi zilianzishwa, zikiwemo Uhominyi- 1941, Balali – 1943, Ukwega – 1943, Ibumu – 1945, Ikokoto – 1946, Lyasa – 1953, Ihimbo – 1954 na Kitowo – 1955. Baadhi ya walimu wa Kiafrika walioshiriki kuanzisha shule hizi ni Yeremia Mlagala, Alexander Nyadzi,  Yoeli Mhoka, Toplas Nsemwa, Enock Mkocha, Yeremia Msola, Allan Chambile, Yoeli Lubazimwa, na Emmanuel Muyula. Kazi ya injili iliyoanzishwa na wamisionari miongoni mwa Wahehe na Wabena iliwezesha kuanzishwa pia kwa zahanati na shule ya Biblia. Kwa mfano, mwaka 1953 zahanati ya kilutheri ya Pommern ilianzishwa na mtaalamu wa mataibabu aitwae Luhangano Badi; na tarehe 3/2/1953 shule ya Biblia ya Kidugala ilianzishwa. Shule hii ilipokea wanafunzi wanane wa kihehe waliokuwa wamepelekwa hapo kwa masomo ya uinjilisti.

Kufika mwaka 1957 eneo la Wahehe lilishakuwa na sharika tano za kilutheri ambazo ni Ihemi, Ilula, Idete na Iringa Mjini na mwaka 1959 uliweka historia ya kipekee kwasababu ni mwaka ambao Kanisa la Kiinjili katika Tanganyika ya kusini lilianzishwa, Kanisa ambalo Rais wake alikuwa Mchg. John Nilsson. Tarehe 6/3/1960 ilikuwa ni siku ya huzuni kwasababu Mchg. Yosefu  Kiwope alifariki dunia na kuzikwa pale Pommern, lakini mwaka uliofuata (yaani 1961) mbinu mpya za kielimu na za kimatibabu ziliwekwa. Kwa juhudi za Kanisa la Kilutheri zaidi zilianzishwa, kama vile shule ya msingi Pommern (1961 chini ya uongozi wa Mwl. Philemon Chambile), na Bomalang’ombe (1963 chini ya uongozi wa Mwl. Abel Chongola). Mwaka 1963 mmisionari Henrik Smedjebacka alichaguliwa kuwa Rais wa Kanisa la Kinjili Tanganyika Sinodi ya Kusini, na mwaka 1964 Zahanati ya Kilutheri Idete ilianzishwa. Mwaka uliofuata 1965 Mchg.Lupumuko Lugala aliteuliwa kuongoza jimbo la Iringa-Uhehe na mwaka 1966 Mchg. Herman Neusberg alizindua rasmi jengo la ibada lililoko Iringa mjini.

Mwaka 1967 Mmisionari Ulla Svenson alifungua rasmi shule ya ufundi ya Kilutheri Mafinga na mwaka huohuo Mchg. Lunogelo Vuhahula alichaguliwa kuwa mkuu wa Jimbo la Iringa – Uhehe. Wakati huU eneo la Uhehe lilikuwa na jumla ya sharika saba, zikiwemo sharika za Ismani na Masisiwe. Mwaka 1969 Mchg.Herman Neuberg alifariki dunia na kuzikwa Pommern na mwaka 1970 Mchg. Allan Chambile alikabidhiwa wajibu wa kuongoza jimbo la Iringa – Uhehe. Jimbo la Iringa lilianza rasmi mwaka 1977 na Mchg.Israel Kiponda alichaguliwa kuliongoza. Kwenye mkutano uliofanyika Lupembe mwaka 1979 palifanywa uamuzi ya kufuata  uongozi wa kiaskofu katika KKKT Sinodi ya Kusini na Katiba ilisomwa kwa mara ya kwanza.

Katiba ilisomwa kwa mara ya pili mwaka 1980 kwenye mkutano uliofanyika Mafinga na majukumu ya Askofu yalikubaliwa rasmi. Kwenye mkutano uliofanyika Makambako mwaka 1981 Mch. Dk. Yuda Kiwovele alichaguliwa kuwa Askofu wa kwanza wa iliyokuwa Sinodi ya Kusini na Mch. Levi Nsemwa alichaguliwa kuwa Msaidizi wa Askofu. Viongozi wengine waliochaguliwa ni Ndg. Obadia Kasumba (Katibu Mkuu) wa Sinodi ya Kusini, Henrick Hult (Mtunza hazina) wa Sinodi na Mch. Nicholas Mwachusi kuwa (Mkuu wa jimbo la Iringa).

Mwaka 1986 ulikuwa na historia ya kipekee kwa kanisa la Kilutheri katika eneo la Iringa. Kwenye mkutano uliofanyika Chimala tarehe 2-7 mwezi Novemba mwaka 1986 Jimbo la Iringa liliagizwa lijiandae kuwa Dayosisi inayojitegemea. Kuhusiana na agizo hili viongozi kadhaa wa Dayosisi iliyokuwa inaandaliwa kutokea walichaguliwa. Baadhi ya viongozi hawa ni Mch. Nicholas Mwachusi, Mchg. Owdenburg Mdegella, Bw. Tuluwene Kulanga na Mwinj. Gerson Munyi. Wakati huo huo Katiba ya Dayosisi mpya ilikamilishwa na kukubaliwa na Mkutano Mkuu wa Dayosisi teule ya Iringa. Wachungaji wa kwanza wenyeji ni Yohana Nyagawa,Joseph Kiwope.Yeremia Mlagala,Lutangilo Mdegela,Iskaka Luvinga na Lupumuko Lugala.[5]

Kikao cha Halmashauri Kuu na cha Mkutano Mkuu wa KKKT vilivyofanyika Arusha na Korogwe mwaka 1986 vilikubali Dayosisi ya Iringa kuanza. Kibali hiki cha KKKT kiliwezesha viongozi rasmi wa Dayosisi mpya ya Iringa kuchaguliwa, kwenye mkutano mkuu uliofanyika tarehe 8/10/1986. Viongozi waliochaguliwa ni Mchg. Owdenburg Mdegella (Askofu mteule), Mch. Nicholous Mwachusi (Msaidizi wa Askofu), Bw. Edward Mnyawami (Katibu mkuu)  na Mwinj. Gerson Munyi (Mtunza hazina).

Baada ya viongozi hawa kuchaguliwa, KKKT Dayosisi ya Iringa ilianza rasmi tarehe 01/01/1987 ikiwa na majimbo matano (Iringa Mjini, Pommern, Idete, Ilula, na Ihemi) na sharika ishirini na nne 24. Askofu Mdegella aliwekwa wakfu kuwa askofu wa kwanza wa Dayosisi ya Iringa tarehe 27/9/1987, siku ambayo Dayosisi hiyo iliingia katika historia kubwa ya kuzinduliwa rasmi na Mch. Nicholas Mwachusi kuingizwa kazini kama msaidizi wa kwanza wa Askofu wa Dayosisi ya Iringa.

Miongoni mwa mambo ya kukumbukwa katika Dayosisi Iringa ni lile la tarehe 20/11/1991 ambapo Dayosisi iliweka historia mpya baada ya kumbariki Mtheolojia Tuseline Kihwele Madembo kuwa mwanamke wa kwanza Mchungaji. Historia hiyo ya kipekee imerudiwa tena mwaka 1998 ambapo. Mch. Agnesi Kulanga amekuwa mkuu wa Jimbo mwanamke wa kwanza katika Dayosisi ya Iringa. Mchungaji Agnes Kulanga ana historia ndefu katika kanisa kwakuwa alishiriki mkutano mkuu wa kwanza wa KKKT mwaka 1963 huko Bukoba uliojadili na kuunganisha makanisa saba na kuunda KKKT. Wakati huo aliwakilisha vijana wa ukanda wa Kusini. Hadi kufikia mwaka 2012 Dayosisi ya Iringa ina wachungaji wanawake 34.[6]

Makao makuu ya Dayosisi ya Iringa yapo mjini Iringa. Kulingana na takwimu za mwaka 2012 Dayosisi ya Iringa ilikuwa na jumla ya sharika sabini na nne (74) zinazounda majimbo saba (7). Majimbo hayo ni Jimbo la Magharibi, Jimbo la Kaskazini, Jimbo la Kaskazini-magharibi, jimbo la Mashariki, Jimbo la Kusini, Jimbo la Kusini- Mashariki na Jimbo la Kusini- Magharibi. Hadi kufikia mwaka 2012 kulikuwa na wakristo wapatao 102,652, wachungaji 168, wainjilisti 496, mitaa 676 na nyumba za ibada 526.[7] Hii ni ishara ya kukua kwa kanisa kwasababu Dayosisi hii ilipoanza mwezi Januari 1987 palikuwepo majimbo matano tu na sharika ishirini na nne tu. Majimbo yaliyokuwepo mwanzoni ni Idete (sharika tano), Pommern (sharika tano), Iringa mjini (sharika nne), Ihemi (sharika nne), Ilula (sharika sita).

Vilevile Dayosisi ya Iringa kufika mwaka wa 2012 imepiga hatua kubwa katika elimu kwa kuwa na chuo kikuu cha Tumaini –Iringa, Chuo cha Uinjilisti kwa wafugaji Ilambilole, shule saba za sekondari ambazo ni Pommerini, Mtera, Malecela, Bomalang’ombe, Ipalamwa, Image na Lutangilo, Kuna shule za awali nne. Pia kuna Hospitali moja ya Dayosisi (Hosptali teule ya wilaya ya Kilolo (DDH). Kuna zahanati 8 ambazo ni Pommerini, Ihimbo, Tungamalenga, Image, Ipalamwa, Idete, Idunda na Ruaha Mbuyuni. Kuna vituo vya Dayosisi ambavyo ni Kituo cha Diakonia, Redio Furaha na Lutheran Centre.[8]

Kuna Idara na vitengo, ambavyo ni Kitengo cha Mahusiano (Bega kwa Bega), Mafunzo, Muziki, na Ukaguzi wa Ndani. Idara zilizopo ni Idara ya Mipango na Maendeleo, Idara ya Uinjilisti na Missioni, Idara ya Vijana na Elimu ya Kikristo. Idara ya Wanawake watoto na Malezi ya Familia, Idara ya Habari na Mawasiliano, Idara ya Utabibu na Diakonia, Idara ya Maandiko na Tafsiri ya Biblia, Idara ya Ufundi Majengo na Viwanja na Idara ya Theolojia kwa Enezi (ETE). [9]

Idara ya ETE imekuwa na mchango mkubwa katika Dayosisi ya Iringa kwa kuelimisha na kuongeza idadi ya watumishi kwenye ngazi ya mtaa na sharika. Ilianzishwa mwaka 1985 katika usharika wa Ihemi. Watumishi ambao wamekuwa wakiandaliwa ni katika ngazi ya wainjilisti, wazee wa kanisa na wakristo raia. Dayosisi ya Iringa iliamua kuanzisha ETE kwa makusudi kwaajili ya kuelimisha watumishi wake. Baba Askofu Dkt. O. Mdegella akishirikiana na wamisionari toka chama cha missioni cha Sweden (Swedish Evangelical Mission – SEM) ndio wanzilishi wa mpango huo. Wamisionari hao ni  Mchg. Stefano Holmstrom aliyepokea wazo na baadaye Mchg. Dkt. Anders Petter Sjodin alipokea na kuendeleza kazi hadi sasa kuna watumishi wengi  ambao wamepitia mafunzo hayo.[10]

Maandiko yaliyochapishwa
  1. KKKT Dayosisi ya Iringa, Toleo maalumu la Jubilee Miaka 100 KKKT Dayosisi ya Iringa (1899-1999): Inter Press of Tanzania, Dar es salaam
  2. KKKT Dayosisi ya Iringa; Miaka 100 ya Injili Uheheni 1899-1999, Wokovu umefika Kwako
3.       Mdegella Yockbeth; From Itonya to Pommern: Historical Development of the First Two Mission Station; BD Research Paper. Makumira, Tanzania 2007.
Taarifa zilizo andikwa
  1. Taarifa ya Maendeleo ya Idara ya Elimu ya Theolojia kwa Enezi (ETE), KKKT Dayosisi ya Iringa, 2012
  2. Takwimu za KKKT Dayosisi ya Iringa (Profile)  2012, Iringa
Mahojiano
  1. Mahojiano na Mchungaji Agnes Kulanga 8/10/2012


VITABU NA MAANDIKO REJEA


[1] Tazama; DIRA, Toleo maalumu la Jubilee Miaka 100 KKKT Dayosisi ya Iringa (1899-1999), 9
[2] Tazama Yockbeth L. Mdegella; From Itonya to Pommern: Historical Development of the First Two Mission Station; BD Research Paper. Makumira, Tanzania 2007.
[3] Tazama KKKT Dayosisi ya Iringa; Miaka 100 ya Injili Uheheni 1899-1999, Wokovu umefika Kwako (Luka 19:9),13.
[4] Tazama, Mwaduma, Dates and Important Events of Iringa Diocese 1899-1999,1
[5] Tazama; DIRA, Toleo maalumu la Jubilee Miaka 100 KKKT Dayosisi ya Iringa (1899-1999), 10.
[6] Tazama Takwimu za KKKT Dayosisi ya Iringa (Profile)  2012; Mahojiano na Mchungaji Agnes Kulanga 8/10/2012
[7] Tazama, Takwimu za KKKT Dayosisi ya Iringa (Profile)   2012.
[8] Ibid
[9] Ibid
[10] Tazama Taarifa ya Idara ya Elimu ya Theolojia kwa Enezi (ETE),KKKT Dayosisi ya Iringa, 2012

WACHUNGAJI WASTAAFU 2012/13

 

 
 

 
















KANISA LA KIINJILI LA KILUTHERI TANZANIA
TAARIFA YA KAMATI YA KICHUNGAJI YA MAASKOFU
ILIYOTOLEWA 15/01/2012 KATIKA KANISA KUU-IRINGA MJINI
TAMKO HII ILISOMWA NA MWENYEKITI WA KAMATI ASKOFU DKT. HANCE MWAKABANA
Utangulizi
Mimi nilipomaliza masomo yangu ya Theoligia  nilianza kazi hapa Iringa wakati huo nikiwa kijana kabisa.Nikiwa masomoni niliandika juu ya Iringa katika andiko langu-kitabu kipo. Wakati ule Iringa mjini ulikuwa usharika mmoja tu na sasa ni sharika nyingi . Hivyo niliyoandika yamekuwa ya kuleta maendeeo na amani katika Kanisa.
Mwaka jana mwezi wa tano tulikuja hapa na baadaye jopo la Maaskofu wa K.K.K.T lilikuja hapa  Iringa na kufanikiwa kukutana  pale katika kituo chetu cha Huruma Centre 10/10/2011. Katika mkutano ile tulizungumza na Wachungaji na baadaye wajumbe Halmashauri Kuu. Patano lilikuwa kamati ile ya maaskofu watatu irudi tena baada ya miezi mitatu ili kuliweka sawa jambo hili, ifanye kazi kama ilivyokuwa imepangwa  awali.
 Siku ya Jumatatu 09/01/2012 sisi watatu tulikutana jioni pale Dar-es-Salaam na siku ya  Jumanne tuliwasili hapa  Iringa.
Ujumbe wetu ulikuwa na
  1. BABA ASKOFU DKT. HANCE MWAKABANA- Mwenyekiti wa Kamati
  2. BABA ASKOFU DKT. MARTIN SHAO- Mjumbe
  3. BABA ASKOFU ELISA BUBERWA -Mjumbe
Jumatano
  • Kukutana na viopngozi waandamizi wa Dayosisi (Managementi)
  •  Kukutana na watumishi wote wa Ofisi Kuu ya Dayosisi mmoja mmoja.
  • Kukutana na Wanachuo Watheolojia na Walimu pia tulikutana nao
Alhamisi
  • Kukutana na Wakristo raia waljitokeza wengi wa kutosha
  • Kukutana na Baba Askofu
  • Kukutana na wenye neno- waliweza kusema kwa uhuru mmoja mmoja na wakati mwingine kundi kwa kundi
Ijumaa
  • Tulikutana na Wachungaji na wajumbe wa Halmashauri Kuu
Jumamosi
  • Kumkutanisha na wenye neno au malalamiko dhidi ya Baba Askofu / Uongozi wa Dayosisi.
  •  Kukutana na Wajumbe wa Halmashauri Kuu Tuliwabadilishia ratiba kama mara nne hivi hivyo tulikutana nao mnano saa 4:30-6:35 usiku
MASWALI/MAMBO MATATU
A.  Picha uliyo nayo ni picha ya namna gani?
B.  Je; umesikia haya yanayosemwa- juu ya Dayosisi?- ndiyo yapo lakini hatujuwi ukweli wake.
-kusaidia turudi katika amani, haya mambo yanatuumiza, turudishe heshima ya Dayosisi yetu.
C.  We kama mwanadayosisi unashauri nini?
-Tufikie mwisho, tupatane, tuyamalize, tupatane
-Kukuwakutanisha wote wenye neno  dhidi ya mwingine tana ana kwa ana tumefanya hivyo.
PATANO
1.  Tumesameheana na yamekwisha
2.  Hatuta chafuana tena ,hatuta lipizana visasi tena
3.  Hatuta oneana tena ,tunataka amani irejee kama awali
4.  Tunataka maombi kama shukrani  kwa Mungu kwa tulipofikia, tuombe toba Mungu kwani kila mmoja wetu amehusika kwa namana moja au nyingine.
5.  Tuendelee kuishi kwa amani katika Dayosisi yetu.

KUNA MAMBO AMBAYO TUMEKUBALIANA YATEKELEZWE NA YATAENDELEA KUFANYWA NA DAYOSISI (UONGOZI WA DAYOSISI).
o   Tunaitangazia Dayosisi nzima kuwa haya mambo yameisha; ahsante Mungu umetufikisha hapa. Tuombe toba na kukiri
o   Naomba nitangaze kwa ujasiri kabisa kuwa mambo yameisha
o   Tusikumbushane vidonda vilivyo pita, tupo mwaka mpya tuanze upya.
o   Kumbukumbu zipo, tusifufue vidonda tena
o   Tuwaambieni wengine pia kuwa haya yameisha .Tuwaambie ndugu zetu na popote tutakapo kwenda na kazi iliyobaki ni kuombeana tu
Tumetoa nafasi ya kutosha kwani tumekuwepo kwa muda wa wiki moja sasa, tumetoa nafasi kwa  kwa wote wenye neno na tumewakutanisha  na wamepatana. Hivyo hatutegemei mtu mwingine kujitokeza  kuamsha na kuanza kusema vinginevyo  tutajua huyo mtu ana nia yake nyingine na haitakii mema Dayosisi na Kanisa letu kwa ujumla.
Tunawaomba ninyi muwe wainjilisti kwa wengine ili warudi nyumbani kwani sasa nyumbani ni salama na shwari hakuna tatizo lingine.Ndugu zangu ya kale yamepita  tyugange yajayo.
Tuwe waangalifu kuto hukumiana kati ya sisi na sisi kwani huwezi juwa mtu mwingine anaweza akawa siyo wa Dayosisi ya Iringa na pengine si Mkristo wa Kanisa la Kiinjili la Tanzania. Tunaamini yameisha kwani kila mmoja amepewa nafasi ya kueleza na kujieleza katika kamati yetu. Tunashukuru kwa ushirikiano na umoja wenu.
Ndimi Mtumishi wenu,
ASKOFU DKT.HANCE MWAKABANA
MWENYEKITI WA KAMATI YA KICHUNGAJI YA MAASKOFU
15/01/2012 


ASKOFU WA  KANISA LA KIINJILI LA KILUTHERI TANZANIA  DAYOSISI YA IRINGA
DKT.O.M MDEGELLA
AZINDUZI WA USHARIKA WA NYAMHANGA
JIMBO  LA  KUSINI  MAGHARIBI(IHEMI)

1. HISTORIA  YA  USHARIKA  WA  NYAMHANGA.

Bwana  Yesu  Asifiwe.

Tunawasalimu  katika  jina  la  Mwokozi  wetu  Yesu  Kristo.

Nyamhanga ilikuwa moja kati ya Mitaa kumi na mbili (12) ya Usharika wa Ipogolo.

Msukumo wa kuanzishwa mtaa wa Nyamhanga ulitokana na mara kwa mara Washarika kukosa huduma za kiroho hasa nyakati za mvua nyingi  ilikuwa vigumu kwa wazee, wagonjwa na watoto kuvuka korongo lililopo kati ya Usharika wa Ipogolo na eneo la  Nyamhanga.

Mwanga ulianza kujitokeza pale mzee wa kanisa Dauson Mbembe alipombatiza ubatizo wa dharura mgonjwa mahututi ndugu Yohana Mnyihanga  tarehe 12/10/1992.

Wakati huo Usharika ulikuwa unaongozwa na Mwinjilisti Yona Kinganga (Kaimu Mchungaji) baada ya Mchg Sawike kuhama.
Kutokana na tukio hilo kaimu Mchungaji alimwomba aliyebatizwa (ndg. Yohana Myihana) nyumba yake itumike kwa sala za asubuhi, alikubali na huduma hiyo ilikaanza  tarehe 15/10/1992.
Huduma zingine ziliendelea kutolewa Usharikani Ipogolo.

Kaimu Mchungaji alipoona maendeleo ya  sala za asubuhi zinaendelea vizuri, aliwaruhusu Washarika waliokuwa wakiishi eneo la Nyamhanga kuanza maandalizi ya kuanzisha mtaa ili huduma za kiroho ziweze kufanyika katika eneo hilo.

Mnamo  mwaka 1993  sala za asubuhi zilihamia nyumbani kwa mzee Mbwilo (Baba Tula ) kukiwa na washarika wanane (08) chini ya uongozi wa mzee wa kanisa Ndugu Dauson  Mbembe.

Uongozi wa maandalizi ya Mtaa huo ulibuni mbinu mbalimbali za kuanzisha Mtaa  ikiwa ni  pamoja  na:-
-          Kuanzishwa kwaya  ya  Upendo ambayo  inaendelea  na  uimbaji  hadi  sasa.
-          Kuwa  na  minada  ya  aina  mbalimbali.
-          Kuanzisha Uinjilisti wa nyumba  kwa nyumba siku za Jumanne na Mikesha ya mara kwa mara.
-          Kuundwa  kwa  kamati  ya majengo.

Kwa  kutumia  mbinu  tajwa  hapo juu tarehe 13/8/1993  tulifanikiwa kununua  kiwanja  chenye ukubwa wa robo tatu eka (3/4) toka  kwa  mzee  Pauli  Kanuru  kwa Tsh  elfu tatu (3,000).Hatua hii  ya  kupata kiwanja iliwasukuma washarika kuanza kukusanya mawe kwa ajili ya  ujenzi  wa  kanisa.
Kiwanja hicho kipo mwambao wa daraja la Cagrielo, hakijapimwa na  kinatumika kama  shamba la viongozi wa kanisa.

Mnamo mwaka 1994  chini ya Mwenyekiti wa majengo Ndugu Awarywa Nnko tulipata kiwanja kilichopimwa.
Kutokana na kupatikana kwa kiwanja hicho uongozi uliamua kanisa  lijengwe katika kiwanja hicho, ndipo washarika walipoanza shughuli za ufyatuaji wa matofali. Tunamshukuru  Mungu kwa kuwatumia watumishi wake Ndugu Awarywa Nnko na Ndugu Chua kusimamia usombaji wa kuni za kuchomea matofali kwa trekta lililotolewa na Shirika la kilimo (EEC).

Trekta hili lilitumiwa pia kipindi hicho kusomba  matofali  ya  awamu  ya  kwanza. Kazi ya ufyatuaji na uchomaji wa matofali ya awamu ya pili zilifanyika mnamo mwaka 1995. Kutokana na mzee Mbwilo kuhamia Makete  sala za asubuhi zilihamishiwa nyumbani  kwa  mzee  Dauson  Mbembe  kuanzia  tarehe  14/7/1995.

Katika kipindi hiki Uongozi uliomba huduma ya shule ya Jumapili (Sunday  School) ianze, uongozi wa Usharika ulikubali na watoto walianza ibada za Shule ya Jumapili tarehe 19/10/1996.
Kazi ya ujenzi wa kanisa ilianza rasmi tarehe 26/9/1996.
Ili kufanikisha ujenzi wa kanisa zilibuniwa mbinu au njia mbalimbali zikiwemo:-
-          Kuanzisha mgahawa.
-          Bahati na sibu iliyotupatia Tsh laki mbili na elfu hamsini (250,000)
-          Wahisani R.C Ipogolo walitupatia Tsh elfu ishirini (20,000).
-          Harambee iliyoongozwa na Mchg Agness Kulanga ilitupatia Tsh laki moja elfu thelathini  (130,000).
-          Makanisa rafiki wa Usharika wa Ipogolo toka Augustana Marekani walitupatia bati sitini (60) gage 28.

Kutokana na Ndugu Awarywa Nnko kupata uhamisho wa kikazi mwaka 1997, Ndugu Mathew Mlangi alichaguliwa kushika nafasi ya Mwenyekiti wa Majengo.
Ndugu Mathew Mlangi  alisimamia kamati hiyo ya Majengo, awamu ya pili ya usombaji wa tofali kwa ajili ya ujenzi wa kanisa.

Ndugu Mathew Mlangi alienda masomoni nje ya nchi, na ndg Henry Mwaipopo alichaguliwa kuchukua nafasi ya uwenyekiti wa majengo, Ili kuharakisha ujenzi wa kanisa unaendelea bila kukwama.
Wakati ujenzi wa Kanisa unaendelea, Uongozi  uliamua, ibada za shule ya Jumapili pamoja na mazoezi ya uimbaji yafanyike kwenye jengo la kanisa lililokuwa linaendelea kujengwa (pagale).

Uongozi wa Mtaa wakati huo ulipata changa moto nyingi kutoka kwa wamiliki wa kiwanja cha kanisa. Kanisa lililazimika kulipa fidia ya Tsh elfu ishirini na tano (25,000) kwa wamiliki wa eneo hilo kwa ajili ya vitindi na mlimao kama ilivyoamuliwa  na  ofisi  ya  Kata ya Kitwiru.

Tunamshukuru sana Mungu kupitia kwa msaidizi wa Askofu wakati huo Mchg Dr Richard Lubava na aliyekuwa Mchg wa Usharika wa Ipogolo Mchg Lusungu Msigwa waliweza kuishawishi ofisi ya bega kwa bega ambayo ilitupatia Tsh Milioni tatu laki nne elfu kumi tatu na mia nne (3,413,400), saruji mifuko mia moja (100), mbao mia moja (100), chokaa mifuko miwili (02) na waya za “Ringbeam”.

Mchango huu pamoja na michango ya washarika ilifanikisha kazi ya ujenzi wa kanisa kukamilika kuta, kupaua na kuchonga  milango.
Shughuli hizi zilifanyika chini ya usimamizi wa mwenyekiti wa majengo Ndugu Henry Mwaipopo na mzee wa kanisa ndugu Dauson Mbembe.
 Kutokana na kukamilika kwa ujenzi wa kanisa tarehe 11/8/2002 ibada zote zilianza kufanyika yamhanga na ukawa mtaa unaojitegemea chini ya uongozi wa mzee wa kanisa Ndugu Dauson Mbembe, kukiwa na waumini sabini na mbili (72).

Huduma ziliendelea chini ya mzee wa kanisa Ndugu Dauson Mbembe  hadi tarehe 30/11/2002 Mtaa ulipopata mwinjilisti, Regina Kibasa. Mtaa ulipopata mwinjilisti, washarika walipata hamasa, na mikakati ya maandalizi ya kuchonga mabenchi, kutengeneza samani za ofisi, kuingiza umeme na maji zilianza.
Michango ya washarika wa Mtaa huu,  pamoja  na  minada  ya  ndani  kazi zote  hizo zilikamilika.
Baada ya Mtaa kukamilisha kazi zilizotajwa hapo juu, lilijitokeza wazo la kujenga nyumba ya mtumishi.

Washarika wa Mtaa huu, kwa michango yao na nguvu kazi wakishirikiana na vijana ishirini na moja (21) toka Usharika wa  Augustana  Marekani walifanikiwa kukamilisha kazi ya kujenga Msingi wa nyumba ya mtumishi.

 Mnamo mwaka 2004, uongozi wa Mtaa uliandaa harambee, na Baba Askofu DKT Owdenburg Moses Mdegella ukiwa mgeni rasmi katika harambee hiyo kwa lengo la kuhamasisha.
Waalikwa wengine walikuwa, Kwaya kuu toka Usharika wa Kanisa Kuu, viongozi  wa kanisa pamoja na viongozi wa Serikali, ndugu na marafiki.
Harambee hii ilichangisha kiasi cha Tsh  laki nane themanini na mbili elfu na mia tatu (882,300/=). Kiasi kilichopatikana katika harambee hiyo  kiliwezesha kukamilisha kazi ya ujenzi wa kuta, kupaua, Milango, kupiga plasta ndani.

Kazi hii ya ujenzi ilifanyika chini ya uongozi wa Mwilisti wa mtaa Regina Kibasa, wachungaji wa Usharika wa Ipogolo, Mchg Abass Tagamtwa na Mchg Nixon Mwitula.
Jengo la kanisa pamoja na nyumba ya mtumishi zilizinduliwa rasmi na Baba Askofu DKT Owdenburg Moses Mdegella tarehe 21/06/2009.

Mtaa wa Nyamhanga hadi kupata hadhi ya  kuwa Usharika umeongozwa na watumishi hawa wafuatao:-
1.     Mzee wa kanisa Dauson Mbembe           11/08/2012 – 30/11/2011
2.     Mwinjilisti Regina Kibasa                                     30/12/2002 – 30/11/2009
3.     Shemasi Regina Kibasa                             01/11/2009 – 14/12/2009 
4.     Shemasi Gaitan Mkemwa             15/12/2009 – 20/09/2011
5.     Mwinjilisti Aneth Mkongwa                      2009 – Hadi sasa ni Mwinjilisti wa
                                                                        Mtaa wa  Stesheni
6.     Mchg Nuru Makweta  -20/9/2011 hadi sasa ni Mchg kiongozi wa Usharika huu mpya.

Makatibu waliotumika hadi kupata Usharika ni hawa wafuatao:-
1.     Vicky Motto -                       2002
2.      Mathias .B. Masele –      2002 - 2006
3.     Noel Chengula  -                2006-Hadi sasa ni Katibu/Mtunza Hazina wa Usharika.

Tunamshukuru Mungu kwa kufanikisha upatikanaji wa  viwanja vinavyoungana na eneo la kanisa.  Viwanja hivi vilipatikana baada ya kanisa kulipa fidia ya Tsh Milioni saba laki moja na nne elfu mia tisa hamsini  (7,104,950/=) kwa waliokuwa wamiliki wa viwanja hivyo tarehe 04/02/2012.

Tunawapongeza  Wazee  wa  kanisa, Kamati ya majengo,Kamati ya ununuzi wa viwanja pamoja na wote  walioshiriki katika kufanikisha upatikanaji wa viwanja hivyo.


Imeandaliwa  na: KAMATI YA MAANDALIZI YA UFUNGUZI WA USHARIKA WA
                                NYAMHANGA:

Tarehe: 12/05/2013


2. RISALA

Baba Askofu wa Dayosisi ya Iringa. Msaidizi wa Askofu. Katibu Mkuu, Wakuu wa Majimbo, Wachungaji Wote, Viongozi wa Serikari na Waumini wote mliohudhuria katika ibada hii,
“ BWANA YESU ASIFIWE”

Baba Askofu.
Kwa niaba ya Washarika wa Usharika Mpya wa Nyamhanga, ambao baada ya muda mfupi ujao utaufungua, awali ya yote napenda kutoa shukurani zangu za dhati, kwanza kwako wewe Baba Askofu, Msaidizi wa Askofu, Katibu Mkuu, Wakuu wa majimbo, Viongozi wa Serikali na wote mliohudhuria katika ibada hii, kwa kumshukuru Mungu kutufikisha  siku ya leo.

Pia napenda kutoa shukurani zangu za dhati kwa Washarika wote wa Usharika wa Ipogolo na Wachungaji wote waliohudumu katika Usharika huo kwa kuuongoza Mtaa wa Nyamhanga hadi kufikia kuwa Usharika, na leo Baba Askofu utaufungua rasmi.
Ningependa Kuwataja  Wachungaji waliohudumu katika Usharika wa Ipogolo, Nyamhanga ukiwa moja wa Mitaa ya Usharika huo. Wachungaji hao ni hawa wafuatao:-

(1)  Mchungaji Agness Kulanga na msaidizi wake Mchg. Aleki Mhanga
(2)  Mchungaji Damian Ngandango
(3)  Mchungaji Lusungu Msigwa
(4)  Mchungaji Abbas Tagamtwa
(5)  Mchungaji Nixon Mwitula (Mchungaji Kiongozi wa Usharika wa Ipogolo hadi sasa) na wasaidizi wake wafuatao;- Mchg. Lunyiliko Muhile, Shemasi Gaitan Mkemwa, Mchg. Lucrecia Mbwilo, na Mchg. Nuru Makweta.
Wote hawa wamefanya kazi kubwa katika kuufikisha Mtaa wa Nyamhanga kuwa Usharika.

Baba Askofu, Mtaa wa Nyamhanga ulianza tarehe 11/08/2002 kwa juhudi za Waumini wa Mtaa huo kwa kushirikiana na Usharika wa Ipogolo.
Wakati Mtaa ulipoanza ulikuwa na Washarika 72, Washarika wamekuwa wakiongezeka siku hadi siku na kufikiaWasharika 1,180 hadi Mtaa ulipofikia kupewa hadhi ya Usharika Mwezi Januari, 2013.

Baba Askofu, kuanzishwa kwa Mtaa wa Nyamhanga ilitokana na Waumini wa Mtaa wa huo na wakazi wa eneo hili kutaka kusogezewa huduma ya Kiroho katika eneo lao, kutokana na kikwazo cha Korongo lililoko kati ya eneo la Nyamhanga na Usharika wa Ipogolo kujaa maji wakati wa masika, Waumini wa eneo la Nyamhanga ilikuwa tatizo kwao kuvuka Korongo hilo na kwenda Ipogolo kuhudhuria Ibada,

Baba Askofu, Usharika huu wa Nyamhanga utakaoufungua leo, umetokana na Usharika wa Ipogolo, Nyamhanga ukiwa Mtaa moja wapo wa Mitaa kumi na mbili (12) ya Usharika huo wa Ipogolo.

Usharika wa Nyamhanga una Mitaa saba (7), Waumini  1,180,  watu wazima ni Waumini  703, kati ya hao, Wanaume ni 266 , na Wanawake ni 439.
Watoto jumla yao ni 485, Wanaume ni 210, na Wanawake ni 275,

Baba Askofu, Usharika wa Nyamhanga una Mitaa Saba (7) kama nilivyokwisha eleza hapo awali, Mitaa hiyo ni:-
(1)  Mtaa wa Stesheni – Nyamhanga una waumini 528
(2)  Mtaa wa Kitwiru  - 174
(3)  Mtaa wa Kibwabwa - 125
(4)  Mtaa wa Lugala - 221
(5)  Mtaa wa Mseke - 65
(6)  Mtaa wa Mosi - 11
(7)  Mtaa wa Isimila – 56

Katika Mitaa hiyo Saba (7), Mitaa Mitatu (3) ni Mitaa ya Mission, Mitaa hiyo ni ifutatayo:-
(1)  Mtaa wa Mseke
(2)  Mtaa wa Mosi
(3)  Mtaa wa Isimila

Baba Askofu, Usharika huu Mpya wa Nyamhanga una Wachungaji Wawili:
(1)  Mchungaji Nuru Makweta – Ambae ni Mchungaji Kiongozi
(2)  Mchungaji Lunyiliko Muhile

Baba Askofu, ninakuahidi kuwa mimi na Mchungaji mwenzangu, tutashirikiana na Waumini wote katika kuifanya kazi yaBWANA katika eneo hili la Usharika huu.
Kufunguliwa kwa Usharika huu wa Nyamhanga, kutaimarisha kueneza neno la Mungu na huduma yake katika eneo hili.

Pili, ni wajibu wa Usharika huu, nikiwa na maana ya Viongozi, Wahudumu na Watenda kazi wote wa Usarika huu wa Nyamhanga kuitangaza Injili kwa watu wote.

Baba Askofu, Usharika wa Nyamhanga pia una Mipango Kazi Kama ifuatavyo:-
(1)  Kazi ya Kiroho:
Kazi kubwa iliyooko mbele yetu ni pamoja na;-
(a)  Kueneza neno la Mungu katika eneo la usharika wa Nyamhanga
(b) Kushirikiana na Viongozi, Wahudumu na Watenda kazi wote wa Usharika katika kuitangaza Injili kwa watu wote, ili waweze kuokolewa kwalo na kumtumikia Mungu.
(c)  Kufanya Uinjilisti wa nyumba kwa nyumba katika eneo hili la Usharika’
(d) Kuimasha na kuendeleza Sel – groups
(e)  Kuandaa semina za neno la Mungu
(f)    Kuandaa Mikutano ya Injili
(g) Kusomesha Wachungaji na Wainjilisti
(h)  Tuna Mipango ya Kutembelea Sharika mbalimbali katika Dayosisi ya Iringa na nje ya Dayosisi kwa kutumia kwaya za Usharika wetu, katika kueneza Injili na pia kujifunza kutoka kwao.
(i)   Kuimarisha huduma za Maombi.

Neno linasema,
                        “BWANA ASIPOIJENGA NYUMBA, WAIJENGAO WAFANYA
                          KAZI  BURE,
                          BWANA ASIPOULINDA MJI YEYE AULINDAYE AKESHA
                          BURE”

        (Zaburi 127: 1)


(2)  Kazi za Kiuchumi:
    Ili kazi ya Kiroho iweze kupata msukumo wa kwenda mbele, tuna Mipango Mkakati ya kazi za Kiuchumi kama ifuatavyo:-
(a)  Kujenga ukumbi
(b) Kujenga Shule ya watoto wadogo (Kindergarten)
(c)  Kujenga Hostel
(d) Kuendeleza Mradi wa upandaji Miti katika shamba lililopo Lugala
(e)  Tuna mpango wa kujenga Maduka ya Biashara kuzunguka eneo la Kanisa
(f)    Pia tuna Mpango wa ujenzi wa shule ya  Ufundi

Mipango hii yote ni endelevu ( Mipango ya muda mrefu).

Baba Askofu,
Mahali popote pale hapakosi changamoto:
Usharika wetu kwa kuwa ndiyo unaanza, tuna changamoto zifuatazo:-
(1)   Usharika una changamoto kubwa ya usafiri, hatuna chombo cha usafiri kwa
ajili ya kuifikia Mitaa yetu ambayo ipo mbali kutoka Makao makuu ya usharika, pamoja na kufanya shughuli zingine za kila siku.

(2)   Tuna upungufu wa Majengo kwa ajili ya ofisi za idara mbali mbali katika
Usharika wetu.

Baba Askofu,
Kwa heshima nakuomba,  karibu ufungue rasmi usharika wa Nyamhanga leo tarehe 12/05/2013.

“BWANA YESU ASIFIWE”

AMEN

NURU MAKWETA
MCHUNGAJI KIONGOZI – USHARIKA WA NYAMHANGA,



                  ASKOFU WA  KANISA LA KIINJILI LA KILUTHERI T ANZANIA
DAYOSISI YA IRINGA

DKT.O.M MDEGELLA

AZINDUZI WA USHARIKA WA NYAMHANGA
MATUKIO KATIKA PICHA

Radio Furaha 96.7 Fm wakifuatilia matukio tayari kurusha moja kwa moja (Live)



Bendi ikitumbuiza tayari kupokea maanadamano


   WAKRISTO WAKIWA TAYARI KWA KUWAPOKEA WAGENI MBALIMBALI AKIWEMO BABA ASKOFU












     MCHUNGAJI NURU AKISOMA RISALA KABLA YA UZINDUZI WA USHARIKA

 MKUU WA JIMBO LA  KUSINI MAGHARIBI(IHEMI) MCHUNGAJI AIKAM CAVALLA AKISOMA NENO 

 KATIBU MKUU BW. NAYMAN CHAVALLA AKISOMA WAJIBU WA USHARIKA KATIKA UFUNGUZI HUO

 BAADHI YA WACHUNGAJI WALIOSHIRIKI KATIKA UZINDUZI HUO
 BABA ASKOFU AKIKAZIA JAMBO KABLA YA KUFUNGUA MLANGO WA KANISA HILO
  MZEE  WA KANISA  BI OTTAVINA MYENZI  AKISOMA MATANGAZO



 WAKRISTO WAKIFUATILIA IBADA HIYO
  WAZEE WAANDAMIZI  WA USHARIKA HUO

 MCHUNGAJI KIONGOZI WA USHARIKA HUO MCHG. NURU MAKWETA AKIWA  TAYARI KWA KAZI

  KWAYA KUU IKITUMBUIZA 








     WAZEE WA KANISA NA WENYEVITI WA KAMATI MBALIMBALI WAKIWA KATIKA PICHA YA PAMOJA 

Monday, May 20, 2013


KWAHERI MAMA MCHUNGAJI ANN KATRIN PERSSON



  Mama tunakushukuru sana kwa mapenzi mema ni maneo ya Baba askofu Dkt. O.M Mdegella wa K.K.K.T-Dayosisi ya Iringa
 "Hongeara mama" ni maneno ya Mchungaji Sara Mdegella kwa mama Ann Katrinn Person

  Mama Mchungaji Runne Persson katikati akiwa na baadhi ya watendakazi wenzake
      Hii ni zawadi yako Mungu akubariki sana
     Ubarikiwe sana 
      Nashukuru sana ni maneo ya mama Mchungaji Runne Persson

       Tunakutakia maisha mema na Mungu akipenda tutaonana


IFUATAYO NI SEHEMU YA HOTUBA YAKE 


Ninawashukuruni sana! Kwanza ninashukuru kwa jioni hii njema kwa ninyi nyote mliofika kwa kuniaga taja…, ni neema ya pekee. Ninashukuru mno! Halafu ninataka kusema asante kwa moyo na upendo mmenionyesha wakati nimekuwepo hapa Iringa, DIRA. Wengine nimekaa nao sana, na wengine tumeonana kwa kifupi tu. Lakini ninataka kusema kwamba ukaribu wenu pamoja na ukarimu umenitia moyo sana na imenisaidia kujisikia kama nipo nyumbani hapa, asanteni sana.
Wenzangu wa ETE, Mchg. Vallence, Mchg. Sarah, Mchg. Ulime na Mary, kama mimi ninavyoona tumefanya kazi vizuri pamoja. Tumepanga kazi,  tumezungumza, tumecheka na tumeomba pamoja ili kazi ya ETE isonge mbele na watu wapate nafasi kumfahamu Mungu wetu anayetaka watu wote wamfahamu  Yesu Kristo katika maisha yake.
Pia ninasema asante Sarah, kwa muda huu tuliokuwa pamoja ofisini na kwenye safari zetu za kuzunguka majimboni kuwaona wenzi wa wachg. na wainj. Umekuwa tayari kunieleza mambo yote ambayo sikuelewa na sikufahamu, na umekuwa tayari kunijibu kila swali. Hii imekuwa msaada mkubwa kwangu na imenisaidia sana katika kazi yangu. Sasa naomba Mungu akubariki katika kazi ya kuchunga Usharika wako, wenzi wa wachungaji na wainjilisti.
Miaka hii michache nimejifunza mengi kutoka kwenu. Na kitu kikubwa hasa nimaana ya maisha ya maombi.
Ninaporudi nyumbani nitaendelea kutoa habari za kazi ya wenzi katika usharika wetu ili wafadhili wenu wapate changamoto kuendelea kujitolea kwa kupitia SEM.
Muda umeenda haraka, miaka 2 ½ imeshapita, na sasa livu yangu imekwisha na nimeitwa kazini nyumbani tena. Mwakani Mungu akipenda, ninataka kufika hapa tena kumtembelea Rune na ninyi nyote, nafikiri Mungu anapenda.
Mungu awabariki ninyi nyote na tutaendelea kuwa pamoja katika maombi, asanteni sana!
UBARIKIO WA MKUU WA JIMBO  ULIOFANYIKA HUKO IHEMI KATIKA PICHA 

 BABA ASKOFU DKT. O.M MDEGELLA AKIWA NA MSAIDIZI WAKE TAYARI KUELEKEA KATIKA IBADA

               MKUU WA JIMBO MTEULE AKIWA TAYARI KATIKA MSTARI TAYARI KUELEKEA KATIKA UBARIKIO WAKE

 KATIBU MKUU BW. NAYMAN CHAVALLA AKIWA NA MKUU WA JIMBO MCHG. AGNES KULANGA


 KATIBU MKUU AKIFURAHIA JAMBO KULIA KWAKE NI BABA ASKOFU DKT. O.M. MDEGELLA
 KWAYA NA BENDI ZIKITUMBUIZA  KUONGOZA MSAFARA KUELEKEA KANISANI

 WAKUU WA MAJIMBO WAKIFUATILIA MATUKIO KATIKA IBADA HIYO
 KATIBU MKUU BW. NAYMAN CHAVALLA NA MTUNZA HAZINA WA DAYOSISI BW. NOEL ILOMO KATIKATI  WAKIFUATILIA JAMBO
 "PONGEZI KWAKO BABA" NI MANENO YA MAMA MCHG. AIKAM CHAVALLA 




HAPA MCHG. AIKAM CHAVALLA AKIWA TAYARI NA VAZI LAKE  RASMI


Tuesday, May 21, 2013


       
          TULIKOTOKA NI MBALI TUMSHUKURU MUNGU

Pichani Baba Askofu Dkt.O.M Mdegella akiwa na Msaidizi wake marehemu mchungaji Nicholaus Chusi mara baada ya kumtambulisha kama  Msaidizi wa Askofu wa Dayosisi ya iringa wanao onekana ni wake zao Mama Askofu ambaye kwa sasa ni Mchungaji Sara Mdegella na Mama Msaidizi wa Askofu Mwalimu Elitha Mkinywa


UBARIKIO WA WACHUNGAJI KUMI NA MASHEMASI 

WATATU KATIKA USHARIKA WA MKWAWA 12.01.2014

No comments

Post a Comment